Hapi Arejesha Gari la Mwalimu Aliyetapeliwa


Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Iringa katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Juni, 2020 imeweza kuokoa kiasi cha fedha zaidi ya shiliingi bilioni 1.2.


Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Iringa, Mweli Kilimali amesema, katika kipindi hicho cha ufuatiliaji wa madeni ya wadaiwa sugu vyama vya akiba na mikopo (SACCOS) 67, vilifikiwa na zaidi ya bilioni 1.2 ziliokolewa.

Mbali na fedha hizo pia amesema kuwa katika opresheni ya kuwatafuta wakopeshaji wa mikopo umiza, wamefanikiwa kukamata  gari lenye namba ya usajili T 311 DDF aina ya Nissan Serena iliyokuwa mali ya mwalimu mstaafu Hadija Nassor Mazola aliyekopa kiasi cha Mil 2 mwaka 2017 kutoka kwa mkopeshaji Micheal Wilson Sanga.

Kwa upande, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi ameipongeza TAKUKURU kwa kazi nzuri ya kuokoa fedha na mali za wananchi.

Comments

Popular posts from this blog

Rais wa Marekani Donald Trump na Makamu Wake Huenda Wakapimwa Tena Corona Baada ya Mtumishi Mwingine Wa IKULU Kukutwa na Virusi Vya Corona

Mchezo wa Kwanza Wapigwa Marekani Bila Mashabiki

Mji mkuu wa Korea Kusini wafunga kumbi za starehe kwa hofu ya Corona